SABATO
“Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana” Zaburi
122:1
Mungu ametupatia siku zote sita za
kutenda mambo yetu, na kuitenga siku moja tu kwa ajli yake. Hii yapaswa kuwa
siku ya baraka kwetu, siku ambayo tunaweka mambo yetu kando na kuelekeza mawazo
yetu kwa Mungu na mbingu. Katika siku hii mioyo yetu inapaswa kuamshwa kwani
tunakutana na Mungu na Kristo mwokozi wetu. Tunaweza kumwona kwa imani. Yeye
anasubiri kurejeza na kubariki kila roho.
Sabato ni wasaa wa Mungu.
Aliibariki na kuitakasa siku ya saba. Aliiweka maalum kwa ajili ya mwanadamu
kuitunza kama siku ya ibada
Tunapaswa kufurahi na kukuza roho
ya ibada ya kweli, roho ya kujiweka wakfu katika siku takatifu ya Bwana.
Tunapaswa kukusanyika pamoja tukiamini kuwa tutapokea faraja na tumaini, nuru
na Amani toka kwa Kristo Yesu.

Amen
ReplyDeleteAmeen!
ReplyDelete